Pichani ni majaji wa shindano hilo.Kutoka kushoto ni Espen Sorensen au maarufu kama Mzungu Kichaa. Yeye alizaliwa nchini Denmark na kisha akakulia Tanzania baada ya kuhamia hapa akiwa na miaka 6 kutokana na wazazi wake kuhamishiwa Tanzania kikazi.Ameshiriki katika harakati za muziki wa Hip Hop nchini Tanzania kwa muda mrefu.Hivi karibuni kwa kushirikiana na Proffessor Jay,alifyatua kibao Jitolee ambacho kilimweka katika chat za muziki kwa namna nyingine kabisa.
Original post @
Star Search 2010
